kahawatungu.com
@kahawatungu Sun, 06 Sep 2026 23:54:03
What Is Kenny Lofton Net Worth?
Kenny Lofton net worth is estimated at $25 million. The former American professional baseball player built his wealth during a 17-year MLB career that saw him play for several teams, including the Cleveland Indians, Atlanta Braves, Chicago White Sox, San Francisco Giants, Pittsburgh Pirates, Chicago Cubs, New York Yankees, Philadelphia Phillies, Los Angeles Dodgers and [...] The post What Is Kenny Lofton Net Worth? appeared first on Kahawatungu.
read morekahawatungu.com
@kahawatungu Mon, 07 Sep 2026 00:03:44
What Is Nick Swisher Net Worth?
Nick Swisher net worth is estimated at $50 million. The retired American professional baseball player built his wealth during a successful MLB career that included a World Series championship with the New York Yankees and an All-Star selection. Swisher played for several MLB teams, including the Oakland Athletics, Chicago White Sox, New York Yankees, Cleveland [...] The post What Is Nick Swisher Net Worth? appeared first on Kahawatungu.
read moretaifaleo.nation.co.ke
@taifaleo Sun, 06 Sep 2026 23:55:59
Rais Ruto asisitiza Kenya haitauza madini ghafi nje ya nchi
RAIS William Ruto amesema Serikali yake inaandaa sera itakayokomesha usafirishaji wa malighafi kutoka Kenya kwenda nje, huku kampuni zikihitajika kuwekeza nchini, kuongeza thamani ya madini na kuunda nafasi za kazi. Akizungumza akiwa Kaunti ya Samburu, wakati wa hafla ya kutoa shukrani ya Katibu wa Ugatuzi, Michael Lenasalon, Rais Ruto alisema amechukua hatua binafsi kuhakikisha usafirishaji wa madini kutoka Magadi unakomeshwa. Alisema sera hiyo itahusu rasilimali zote za nchi, zikiwemo mafuta, dhahabu na madini adimu. "Kuanzia sasa, msimamo wetu wa kisera ni kwamba iwe ni soda ya Magadi, mafuta au madini yetu yote, ikiwemo dhahabu na madini adimu, tumeamua kwamba hatutasafirisha tena malighafi," alisema. Rais alisema Serikali itahakikisha madini yanachakatwa nchini ili kuongeza thamani na kutoa ajira kwa Wakenya. Alisema pia Serikali inashirikiana na mfanyabiashara Aliko Dangote kuanzisha kiwanda cha kusafisha mafuta Lamu. Aidha, alisema Serikali inashirikiana na wawekezaji wengine kuanzisha viwanda vya kusafisha dhahabu na kuchakata madini katika maeneo mbalimbali nchini. "Itakuwa si busara kwa Serikali kusafirisha malighafi, kuunda ajira na kuongeza thamani katika nchi nyingine wakati tuna vijana wengi wanaohitaji ajira," alisema. Rais alisema alilazimika kwenda Kajiado kushughulikia mkataba wa awali wa uchimbaji, ambao alisema ulikuwa ukinufaisha zaidi kampuni kuliko Wakenya. Alisema mkataba huo, ambapo Kenya ilipata asilimia tano pekee huku asilimia 95 ya thamani ikitengenezwa nje ya nchi, umefutwa. "Hatuwezi kufuata malighafi zetu nje ya nchi na kununua bidhaa kwa bei ya juu huku vijana wetu wakikosa ajira," alisema. Rais alisema tenda mpya itatangazwa na kampuni zaidi zitaruhusiwa kuwekeza Kajiado. Alisema Serikali haitaki kampuni moja pekee, bali inataka zaidi ya kampuni tano na hata 10 zitumie rasilimali hizo kuunda ajira na kuongeza thamani. Jumamosi, Rais alitangaza kuwa mkataba wa uchimbaji wa Tata Chemicals, iliyojulikana zamani kama Magadi Soda, utatangazwa upya kupitia zabuni yenye ushindani. Alisema mkataba huo ulikuwa wa kunyanyasa Kenya na hauwezi kuendelea. Rais Ruto pia aliahidi kuhakikisha ushirikiano wa kisiasa kati ya UDA na ODM unaendelea hata baada ya uchaguzi wa 2027. Alishukuru ODM kwa kusaidia kupunguza joto la kisiasa nchini.
read morestandardmedia.co.ke
@standard Mon, 07 Sep 2026 00:00:00
Four dead, scores injured and vehicles torched: How horrific Homa Bay attack on Sifuna team was planned
A Standard investigation alleges that political leaders, youths and police officers were involved in planning and executing the violent disruption of the Linda Mwananchi convoy in Homa Bay.
read morekahawatungu.com
@kahawatungu Sun, 06 Sep 2026 22:52:10
Dr James Mworia appointed National Infrastructure Fund CEO
Dr James Mworia has been appointed the founding Chief Executive Officer of the National Infrastructure Fund (NIF), with the appointment taking effect on September 7, 2026. The NIF Board said Mworia was selected following a competitive recruitment process to lead the newly established fund and oversee the implementation of its mandate. The appointment comes as [...] The post Dr James Mworia appointed National Infrastructure Fund CEO appeared first on Kahawatungu.
read moretaifaleo.nation.co.ke
@taifaleo Sun, 06 Sep 2026 22:55:41
Nyoro:Tutamshinda Ruto kura ya 2027 na kuokoa nchi
KIONGOZI wa People's Party, Ndindi Nyoro amesema yuko tayari kuwania urais mwaka 2027 chini ya muungano wa upinzani, akisema ana uwezo wa kumshinda Rais William Ruto. Bw Nyoro alisema Jumapili kwamba iwapo muungano huo utamteua kuwa mgombea wake wa urais, atakabiliana na Rais Ruto katika uchaguzi mkuu ujao. "Ninafaa kuwa Rais wa Kenya," alisema Bw Nyoro alipohutubia mikutano ya hadhara katika maeneo ya Kangaita na Mukinduri, Kaunti ya Kirinyaga. Alisema adui wa pamoja wa vyama vya upinzani ni Rais Ruto na akaahidi kwamba iwapo atateuliwa, atamshinda na kumrudisha nyumbani kwake Sugoi. "Ikiwa muungano wa upinzani utakubaliana kwamba mimi ndiye mgombea wa kuwania urais dhidi ya Ruto, nitapambana naye na kumshinda," alisema. Bw Nyoro alijigamba kuwa ana rekodi ya kuchapa kazi na akasema akipewa nafasi ya kuongoza Kenya, anaweza kubadilisha maisha ya wananchi ndani ya mwaka mmoja. Alitaja miradi ya elimu katika eneo lake la uchaguzi kama mfano wa uwezo wake wa kuleta mabadiliko. "Katika eneo langu nimehakikisha hali katika shule za upili ni nzuri. Wanafunzi hulipa Sh500 pekee kwa muhula na chakula hutolewa bila malipo," alisema. Aliongeza kuwa ameboresha shule za msingi za umma na mazingira kwa wanafunzi. "Mimi ni mchapa kazi na ninapaswa kupewa nafasi ya kuongoza Kenya kwa manufaa ya Wakenya wote," alisema. Bw Nyoro pia alionyesha matumaini kwamba vyama vya upinzani vitaafikiana na kuteua mgombea mmoja wa urais.
read moretaifaleo.nation.co.ke
@taifaleo Sun, 06 Sep 2026 21:55:35
Wantam! Gachagua ainua mkono, asema Sifuna tosha kupambana na Ruto 2027
ALIYEKUWA Naibu rais Rigathi Gachagua amefungua mlango wa muungano usiotarajiwa wa kisiasa kati ya Mlima Kenya na Seneta wa Nairobi Edwin Sifuna, akisema eneo hilo liko tayari kumuunga mkono iwapo atachaguliwa kuwa mgombea wa pamoja wa upinzani katika uchaguzi wa 2027. Katika hatua inayotofautiana na siasa za viongozi wa kikanda zinazoshuhudiwa kwa sasa, Bw Gachagua alisema yuko tayari kuwa mgombea mwenza wa Bw Sifuna au kumruhusu seneta huyo kuwa naibu wake, iwapo hilo litasaidia kumng'oa Rais William Ruto madarakani. "Niko tayari hata kuwa naibu wake. Yeye pia anaweza kuwa naibu wangu. Sifuna ni mshirika sawa katika mpango wa upinzani kutafuta mgombea urais wa pamoja," alisema Bw Gachagua alipohutubia Wakenya mjini Spokane, Amerika, Jumamosi jioni. Alisema upinzani haupaswi kuharakisha kumteua mgombea wake wa urais, akipendekeza uamuzi huo ufanywe kati ya Machi na Mei mwakani. "Hakuna haraka. Tutahakikisha tutamshinda Rais Ruto katika awamu ya kwanza ya uchaguzi," alisema. Kauli hizo ni ishara ya wazi kwamba Bw Gachagua yuko tayari kuangalia nje ya Mlima Kenya katika kutafuta nguvu za kisiasa za kukabiliana na Dkt Ruto. Kwa miezi kadhaa, Bw Gachagua amejitokeza kama mmoja wa viongozi wakuu wa kisiasa wa Mlima Kenya, baada ya kutofautiana vikali na Rais Ruto. Hata hivyo, msimamo wake wa sasa unaashiria kuwa mkakati wake unaweza kuwa mpana zaidi ya kutafuta tiketi ya upinzani. Anataka pia kuhakikisha kura za Mlima Kenya zitatumika katika muungano mpana wa upinzani wenye uwezo wa kumshinda Dkt Ruto badala ya eneo hilo kujitenga kwenye uchaguzi mkuu wa 2027. Bw Gachagua alipuuzilia mbali hoja kwamba Bw Sifuna hawezi kuungwa mkono Mlima Kenya kwa sababu anatoka magharibi mwa Kenya. Alimlenga Kiongozi wa Wengi katika Seneti Aaron Cheruiyot, ambaye amekuwa akihoji ikiwa Mlima Kenya utamuunga mkono Bw Sifuna iwapo atapewa tiketi ya upinzani. Bw Gachagua alikumbusha kwamba Mlima Kenya ulimuunga mkono kwa wingi Dkt Ruto katika uchaguzi wa 2022, licha ya Rais huyo kutotoka eneo hilo. "Wachache walimpigia kura Raila Odinga. Wote wawili hawakuwa watu wa mlima," alisema. Pia alikataa hoja ya Katibu Mkuu wa COTU Francis Atwoli kwamba Bw Sifuna ni mchanga mno kuwa rais. Bw Gachagua alimtaja aliyekuwa Rais wa Amerika Barack Obama, aliyechaguliwa akiwa na miaka 47, akisema umri haupaswi kutumiwa kuwazuia wanasiasa vijana kuwania urais. "Ikiwa Obama alichaguliwa kuongoza taifa lenye nguvu zaidi duniani akiwa na miaka 47 mwaka 2008, ni nini kinachomzuia Sifuna kuchaguliwa kuwa Rais wa Kenya akiwa na miaka 45 mwaka 2027?" aliuliza. Bw Gachagua amesema mara kwa mara kuwa ushindani wa upinzani dhidi ya Dkt Ruto ni suala la kuunganisha kura kuliko tamaa za mtu mmoja mmoja. "Niko tayari kumuunga mkono mgombea mwingine yeyote isipokuwa Rais Ruto mwaka 2027," alisema. Msimamo huo unaweza kuwa muhimu vyama vya upinzani vinapojadiliana kuhusu tiketi ya pamoja. Bw Gachagua anajenga DCP kuwa chama cha kitaifa, huku aliyekuwa Waziri wa Usalama wa Ndani Fred Matiang'i akiwa na tiketi ya Jubilee. Bw Sifuna naye amejitokeza kama mmoja wa wanasiasa vijana wenye sauti katika kundi la Linda Mwananchi. Viongozi wengine wa upinzani, akiwemo aliyekuwa Naibu Rais Kalonzo Musyoka na kiongozi wa Narc-Kenya Martha Karua, pia wanatajwa katika mazungumzo kuhusu muundo wa muungano wa 2027. Bw Gachagua pia aliitaka IEBC kuhakikisha uchaguzi wa 2027 unaaminika, hasa katika ununuzi wa vifaa, teknolojia na usimamizi wa mchakato wa uchaguzi.
read morekahawatungu.com
@kahawatungu Sun, 06 Sep 2026 16:09:19
Senior Kenya Prisons officer found dead in car in Juja
A senior Kenya Prisons Service officer was found dead inside his car at an open field behind Spur Mall in Juja, Kiambu County. Eric Kiarie Wainaina, a 40-year-old Senior Superintendent of Prisons (SSP) attached to the Kenya Prisons Service Central Region Headquarters in Nyeri, was found unresponsive on Sunday morning. Police said a member of [...] The post Senior Kenya Prisons officer found dead in car in Juja appeared first on Kahawatungu.
read morekahawatungu.com
@kahawatungu Sun, 06 Sep 2026 15:56:34
When the springs run dry: Drought pushes Kisii families to the brink
At dawn in Nyamesocho, Masaba South, the quiet of the countryside is increasingly broken by raised voices at the Rianyabicha water springs. For years, the springs have been a lifeline for families in the area. But as a prolonged dry spell tightens its grip, the precious commodity has become a source of tension — and, [...] The post When the springs run dry: Drought pushes Kisii families to the brink appeared first on Kahawatungu.
read morekahawatungu.com
@kahawatungu Sun, 06 Sep 2026 16:00:14
Mysterious 'Virgin Mary' image draws thousands to Kisii village
It began with an ordinary wall. There was nothing remarkable about the wall at a modest home in Emenwa village, Nyamache, Bobasi, Kisii County—until villagers began claiming they could see the unmistakable outline of a woman on it. Then came the whispers. "It looks like Mary." Within hours, word had spread from one homestead to [...] The post Mysterious 'Virgin Mary' image draws thousands to Kisii village appeared first on Kahawatungu.
read morekahawatungu.com
@kahawatungu Sun, 06 Sep 2026 16:04:22
Volcano eruption leaves 170,000 passengers stranded in Indonesia
Around 170,000 passengers have been left stranded after a volcanic eruption forced Indonesian authorities to temporarily suspend operations at eight airports. Jakartas Soekarno-Hatta International Airport was the first to be closed on Sunday morning after ash from Anak Krakatau was detected in airspace near the airport. The transport ministry said 1,558 flights have been delayed [...] The post Volcano eruption leaves 170,000 passengers stranded in Indonesia appeared first on Kahawatungu.
read morestandardmedia.co.ke
@standard Sun, 06 Sep 2026 16:00:00
Echoes of shame: Inside the planning of horrific Homa Bay attack on Sifuna team
A Standard investigation alleges that political leaders, youths and police officers were involved in planning and executing the violent disruption of the Linda Mwananchi convoy in Homa Bay.
read moreRight Column Content