taifaleo.nation.co.ke
@taifaleo Tue, 07 Jul 2026 02:55:46
IEBC yafufua mpango wa kupimia wanasiasa pesa za kampeni
TUME Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) imefufua mpango wake wa kudhibiti matumizi ya fedha katika kampeni za uchaguzi kwa kuchapisha rasimu ya kanuni mpya zinazolenga kuweka kiasi cha matumizi ya wagombea na vyama vya kisiasa katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2027. Katika rasimu hiyo iliyochapishwa Jumatatu, Julai 6, 2026, IEBC imependekeza kuwa mgombea urais asitumie zaidi ya Sh4.44 bilioni katika kampeni zake, huku matumizi ya chama cha kisiasa yakipangwa kutozidi Sh17.7 bilioni. Kwa mujibu wa mapendekezo hayo, wagombea wa ugavana, useneta na uwakilishi wa wanawake wataruhusiwa kutumia kati ya Sh12.3 milioni na Sh123 milioni, kutegemea ukubwa wa kaunti na idadi ya wakazi. Wanaowania ubunge watatumia kati ya Sh17.5 milioni na Sh123 milioni, huku wanaowania uwakilishi wa wadi katika mabunge ya kaunti wakiruhusiwa kutumia kati ya Sh2.5 milioni na Sh20 milioni kulingana na ukubwa na idadi ya wakazi wa wadi husika. Hii ni mara ya pili kwa IEBC kujaribu kudhibiti matumizi ya fedha za kampeni baada ya juhudi za mwaka 2016 kugonga mwamba. Wakati huo, Bunge lilisitisha utekelezaji wa kanuni hizo kwa kurekebisha Sheria ya Ufadhili wa Kampeni za Uchaguzi na kuahirisha utekelezaji wake hadi baada ya uchaguzi wa mwaka 2017. Uwajibikaji Mwenyekiti wa IEBC Erastus Ethekon amesema kanuni hizo zinalenga kuimarisha uwajibikaji na uwazi katika usimamizi wa fedha za kampeni. "Kanuni hizi zinakusudia kuimarisha uwajibikaji katika usimamizi wa fedha za kampeni za wagombeaji na vyama vya kisiasa," alisema Bw Ethekon. Alisema Sheria ya Ufadhili wa Kampeni za Uchaguzi ya mwaka 2013 inapatia IEBC mamlaka ya kuweka viwango vya michango, matumizi na kusimamia uwajibikaji wa fedha za kampeni. IEBC pia imewapa Wakenya hadi Julai 15, 2026 kuwasilisha maoni yao kuhusu rasimu hiyo kabla ya kanuni hizo kuidhinishwa. Wakati huo huo, tume hiyo imekumbusha wadau kuhusu ratiba ya maandalizi ya uchaguzi wa mwaka 2027. Kwa mujibu wa ratiba hiyo, maafisa wa umma wanaonuia kugombea viti watalazimika kujiuzulu ifikapo Februari 9, 2027, miezi sita kabla ya uchaguzi. Vyama vya kisiasa vitapaswa kuwasilisha orodha ya wanachama na majina ya wanaotaka kushiriki kura za mchujo ifikapo Machi 16, 2027, huku mchujo wa vyama ukitarajiwa kukamilika ifikapo Mei 9, 2027. Uteuzi rasmi wa wagombea wa vyama na wawaniaji huru utafanyika kati ya Mei 29 na Juni 11, 2027, huku malalamishi yote yanayohusu uteuzi yakitakiwa kuwasilishwa kwa IEBC kabla ya Juni 12, 2027. Hatua ya IEBC ya kupendekeza kiwango cha pesa za matumizi ya kampeni inajiri wakati ambapo wanasiasa wengi wamekuwa wakitumia mabilioni ya fedha katika shughuli za uwezeshaji wa wananchi, ambazo zimekuwa zikitafsiriwa kama kampeni za mapema kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka ujao.
read morekahawatungu.com
@kahawatungu Tue, 07 Jul 2026 02:32:33
Kipenzi Sugar Plans Sh1.45 Billion Factory in Siaya to Boost Sugar Production
Kipenzi Sugar Limited plans to invest Sh1.45 billion in the construction of a sugar factory in Mur Malanga, Siaya County, in a move expected to increase local sugar production, create jobs and provide a ready market for sugarcane farmers. According to an Environmental Impact Assessment (EIA) report submitted to the National Environment Management Authority (NEMA), [...] The post Kipenzi Sugar Plans Sh1.45 Billion Factory in Siaya to Boost Sugar Production appeared first on Kahawatungu.
read morekahawatungu.com
@kahawatungu Tue, 07 Jul 2026 02:46:47
Kenya's Steel Mills Operating at Just 36% Capacity Despite Construction Boom, Manufacturers Say
A large share of Kenyas steel production capacity remains idle despite rising demand driven by infrastructure projects and the governments affordable housing programme, with manufacturers blaming high production costs, cheap imports and inconsistent tax policies. The Kenya Association of Manufacturers (KAM) says local steel mills are operating at only 36 percent of their installed production [...] The post Kenyas Steel Mills Operating at Just 36% Capacity Despite Construction Boom, Manufacturers Say appeared first on Kahawatungu.
read morekahawatungu.com
@kahawatungu Tue, 07 Jul 2026 02:09:09
Woman arrested after boyfriend fatally stabbed in Embakasi
A 26-year-old woman was arrested after her boyfriend was allegedly stabbed to death following a domestic dispute in Nairobi's Embakasi area. According to police, the incident was reported at about 9.40pm on Monday at Villa Police Station. Police responded to the scene and found the body of 30-year-old Brian Mwakha lying in a pool of [...] The post Woman arrested after boyfriend fatally stabbed in Embakasi appeared first on Kahawatungu.
read morekahawatungu.com
@kahawatungu Tue, 07 Jul 2026 02:13:41
18 Chinese nationals arrested in Nairobi over suspected cyber fraud
At least 18 Chinese nationals were arrested following a major operation targeting a suspected cyber fraud syndicate operating from an apartment in Nairobi's Kilimani area. The operation was conducted on Monday afternoon by detectives from the Directorate of Criminal Investigations (DCI) based at Kilimani, working alongside officials from the Chinese Embassy. According to police, the [...] The post 18 Chinese nationals arrested in Nairobi over suspected cyber fraud appeared first on Kahawatungu.
read moretaifaleo.nation.co.ke
@taifaleo Tue, 07 Jul 2026 01:55:13
Kampeni zachacha Ol Kalou zikibaki siku 10 kura zipigwe
HUKU zikisalia siku kumi pekee kabla ya uchaguzi mdogo wa ubunge wa Ol Kalou, ushindani huo umegeuka kuwa kipimo cha nguvu za kisiasa katika eneo la Mlima Kenya kuelekea Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2027. Mirengo inayoshindana imetaja uchaguzi huo kama kura ya maamuzi kuhusu mwelekeo wa kisiasa wa eneo hilo, huku kila upande ukitaka kuthibitisha kuwa unaungwa mkono na wapigakura wengi. Wagombeaji wanaopigiwa upatu ni Douglas Waweru wa chama cha Democracy for Citizens Party (DCP), Muchina Nyaga wa chama tawala cha United Democratic Alliance (UDA) na Wilson Kigwa wa Jubilee. [caption id="attachment_189827" align="alignnone" width="2000"] Mgombeaji kiti cha Ol Kalou kwa tikiti ya UDA Samuel Muchina Nyagah akipokezwa cheti cha uteuzi na Katibu Mkuu Hassan Omar mnamo Mei. Picha|Boniface Bogita[/caption] Wengine sita pia wanawania kiti hicho. Kiti hicho kilibaki wazi baada ya kifo cha Njuguna Kiaraho wa chama cha Jubilee mnamo Machi 29, 2026. Mgombeaji wa Jubilee, Bw Kigwa, anakabiliwa na changamoto baada ya kiongozi wa chama hicho, rais mstaafu Uhuru Kenyatta, na mgombea wake wa urais Dkt Fred Matiang'i, kutoshiriki kampeni zake. Aidha, Mbunge Mteule wa Jubilee Sabina Chege ameasi chama chake na sasa anamuunga mkono mgombeaji wa UDA. Uchaguzi huo umegeuka kuwa pambano kati ya serikali ya Rais William Ruto na upinzani unaoongozwa na aliyekuwa Naibu Rais Rigathi Gachagua. Bw Gachagua ametangaza kuwa atafanya kampeni Ol Kalou kwa siku tatu kuanzia Julai 10 kabla ya kampeni kufungwa Julai 13. Nyumba ya Seneta wa Nyandarua John Methu katika kijiji cha Mugumo imekuwa kituo cha mikutano ya kisiasa ya wafuasi wa Bw Gachagua, huku viongozi wa serikali wakifanya ziara mbalimbali za maendeleo wakiahidi miradi ili kuvutia wapigakura. Kati ya wagombeaji tisa, ni Bw Nyaga pekee anayemuunga mkono waziwazi Rais Ruto na serikali ya UDA, huku wengine wakiwa upande wa upinzani. Katika mdahalo uliopeperushwa na Inooro TV Julai 5, Bw Nyaga alikabiliwa na mashambulizi kutoka kwa wagombeaji wengine lakini alitetea sera zake. Bw Gachagua amesema idadi kubwa ya wagombea ni ishara ya demokrasia na kwamba hakuna anayepaswa kuzuiwa kugombea. Hata hivyo, wachambuzi wa siasa wanaonya kuwa Bw Gachagua ndiye anayehatarisha zaidi kisiasa iwapo mgombea anayemuunga mkono atashindwa, kwani hali hiyo itadhoofisha madai yake ya kuwa kinara wa kisiasa wa Mlima Kenya na kuathiri azma yake ya kuwania urais mwaka 2027. Kwa upande mwingine, Naibu Rais Kithure Kindiki amesema ushindi wa UDA katika uchaguzi huo utathibitisha kuwa siasa za ubaguzi na kujitenga hazina nafasi katika eneo la Mlima Kenya. Shinikizo pia linaongezeka kwa Prof Kindiki kushiriki moja kwa moja katika kampeni hizo, huku matokeo yakitarajiwa kuathiri nafasi yake ya kuendelea kuwa mgombea mwenza wa Rais Ruto mwaka 2027. Mbunge wa Laikipia Mashariki Mwangi Kiunjuri, ambaye ni mmoja wa viongozi wanaompigia debe mgombea wa UDA, alisema chama hicho kina uhakika wa kushinda. "Tunaendelea vizuri na takwimu zetu zinaonyesha tutashinda. mgombea wetu ndiye bora," alisema. Lakini Mbunge wa Kipipiri Wanjiku Muhia, anayemuunga mkono Bw Gachagua, alisema mgombea wa DCP ndiye anayeongoza. Alisema uchaguzi huo unalenga kuthibitisha kuwa eneo la Mlima Kenya linaweza kufanya maamuzi yake ya kisiasa bila kushinikizwa. Mchambuzi wa siasa Malila Munywoki amesema uchaguzi huo utakuwa mtihani muhimu kwa Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) na Idara za usalama kuonyesha vinaweza kusimamia uchaguzi huru, wa haki na wa amani kabla ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2027. Naye Gavana wa Nyandarua Kiarie Badilisha hajaweka wazi mgombeaji anayemuunga mkono, lakini amekuwa akiwaambia wakazi kuwa kisiasa yuko upande ambao wananchi wengi wa kaunti hiyo wanaunga mkono, kauli ambayo imezua uvumi kuwa huenda akahama chama kabla ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2027.
read morekenyans.co.ke
@kenyans Tue, 07 Jul 2026 01:20:45
KeNHA Sets New Toll Rate for Gilgil-Mau Summit Section of Nairobi-Nakuru Road
Once completed, the highway will improve traffic flow, reduce travel times and vehicle operating costs, and strengthen connectivity between Nairobi and Nakuru counties.
read morekahawatungu.com
@kahawatungu Tue, 07 Jul 2026 01:38:24
List of Accredited Institutions Offering Law Courses in Kenya for 2026
The Council of Legal Education (CLE) has released the official list of accredited institutions licensed to offer law programmes in Kenya for the 2026 academic year, while also identifying universities with pending applications for accreditation. In a notice issued on Tuesday, July 7, 2026, the Councils Chief Executive Officer, Prof. Busalile Jack Mwimali, said only [...] The post List of Accredited Institutions Offering Law Courses in Kenya for 2026 appeared first on Kahawatungu.
read morestandardmedia.co.ke
@standard Tue, 07 Jul 2026 01:20:00
Prison heist: How rogue payroll clerk transferred Sh41 million
The DCI has launched investigations into a Sh42 million Kenya Prisons payroll fraud in which rogue transfers were made to nearly 1,000 officers using compromised payroll credentials.
read morekahawatungu.com
@kahawatungu Tue, 07 Jul 2026 01:00:03
KFS Invites Public Views on Proposed Airstrip at Upper Imenti Forest
The Kenya Forest Service (KFS) has invited members of the public and stakeholders to submit views on a proposal to construct an airstrip and related infrastructure at Upper Imenti Forest in Meru County. In a notice issued on Tuesday, July 7, 2026, KFS said the project, which will be located at the Meru Forest Station, [...] The post KFS Invites Public Views on Proposed Airstrip at Upper Imenti Forest appeared first on Kahawatungu.
read moreRight Column Content