kahawatungu.com
@kahawatungu Wed, 15 Jul 2026 01:15:07
Discovery of 50 old graves in Marsabit sparks historical investigation
Authorities in Marsabit County launched investigations after the discovery of approximately 50 old graves in Korole area near the Chalbi Desert, a site believed to hold significant historical importance. The graves were discovered on Tuesday afternoon by a herdsman grazing livestock in Mbagasi Village, Kambinye Sub-location, Kargi Location, within Laisamis Constituency. Police officers visited the [...] The post Discovery of 50 old graves in Marsabit sparks historical investigation appeared first on Kahawatungu.
read morekahawatungu.com
@kahawatungu Wed, 15 Jul 2026 01:17:11
How to Buy Airtime from TymeBank
Buying airtime from your TymeBank account is a quick and convenient way to recharge your mobile phone without visiting a shop. Using the TymeBank app, you can purchase airtime for yourself or someone else at any time, provided you have sufficient funds in your account. Learning how to buy airtime from TymeBank helps you stay [...] The post How to Buy Airtime from TymeBank appeared first on Kahawatungu.
read morekahawatungu.com
@kahawatungu Wed, 15 Jul 2026 01:18:20
Grade three pupil killed after tree branch falls at Kiambu school
An eight-year-old Grade Three pupil died after a dry tree branch fell on her while she was having lunch at Muchatta Primary School in Kiambaa Sub-County, Kiambu County. The tragic incident occurred on Tuesday afternoon. According to police, pupils were seated under a tree within the school compound during the lunch break when a dry [...] The post Grade three pupil killed after tree branch falls at Kiambu school appeared first on Kahawatungu.
read moretaifaleo.nation.co.ke
@taifaleo Wed, 15 Jul 2026 00:55:49
Rais wa zamani wa soka Nick Mwendwa anavyomudu kufuga kuku 150,000 wa kienyeji
KILA siku mayai zaidi ya 2,500 huwekwa kwenye kitotoa, mamia ya vifaranga wanaanguliwa kila baada ya siku 21, huku wafanyakazi wakikesha kuhakikisha zaidi ya kuku 150,000 wa kienyeji wanapata chakula, maji na uangalizi unaohitajika. Hivi ndivyo Nick Mwendwa, aliyewahi kuongoza Shirikisho la Soka Kenya (FKF), anavyosimamia moja ya mashamba makubwa zaidi ya kuku halisi wa kienyeji nchini katika eneo la Kalii mjini Makindu, Kaunti ya Makueni. Kilichoanza miaka mitatu iliyopita kwa kuku saba waliokuwa wa mamake, sasa kimegeuka kuwa mradi mkubwa wa ufugaji unaotegemea teknolojia ya kisasa. Safari hii ya kuwekeza katika kuku wa kienyeji haijakuwa rahisi. "Sikuwa na ujuzi wowote wa ufugaji kuku. Nilikumbwa na changamoto si haba ikiwemo kiwango duni cha kuanguliwa kwa mayai, gharama kubwa ya lishe, na kupotea kwa umeme kila mara ambako kulitishia uzalishaji," Mwendwa anaambia Akili Mali tulipotembelea mradi huo. [caption id="attachment_190105" align="alignnone" width="2560"] Rais wa zamani wa FKF Nick Mwendwa akiokota mayai shambani mwake Makueni. Picha|Evans Habil[/caption] Changamoto kuu ambayo nusra izime ndoto yake ni kupoteza vifaranga wapatao 500 kutokana na sababu ya kukosa ufahamu wa jinsi ya kuchanganya chakula chao. Mwendwa anasema wazo la kuingilia ufugaji halikutokana na mapenzi ya kilimo, bali baada ya kushindwa kupata kuku halisi wa kienyeji katika maduka makubwa. "Niligundua mahitaji yalikuwa makubwa kuliko uzalishaji. Wakulima wengi walikuwa wamehamia kufuga aina ya kuku walioboreshwa (layers na broilers), lakini walaji bado wanataka ladha ya kuku halisi wa kienyeji," anasema. Baada ya kufanya utafiti katika masoko ya Ukambani, alibaini kuwa madalali walikuwa wakinunua kila kuku wa kienyeji aliyeletwa sokoni na kuwapeleka Nairobi, jambo lililodhihirisha gapu kubwa ya biashara hiyo. Hapo ndipo alipoanza mradi wake kwa kuku saba waliokuwa wa mamake. "Niliwatenga na kuamua kizazi chote kitokane na hao pekee ili kuhifadhi uhalisia wa mbegu," anaelezea. Mwanzoni, hata wazazi wake hawakuamini ndoto yake. "Mamangu alicheka niliposema nataka kufikisha kuku 15,000. Baadaye nilipoweka lengo la kuku milioni moja, baba alisema Nairobi imenichanganya," akaambia 'Akilimali' shambani mwaki eneo la Kalii, Makindu huku akitabasamu. Changamoto nyingine ilianza baada ya mayai karibu 450 kushindwa kuanguliwa, hali iliyomlazimu kununua mashine ya kwanza ya kuatamia mayai. [caption id="attachment_190106" align="alignnone" width="2560"] Mwendwa akionyesha mayai yaliyotagwa katika shamba lake la kuku Makueni. Picha|Evans Habil[/caption] Matokeo ya awali hayakuridhisha kwani ni asilimia 41 pekee ya mayai yaliyoanguliwa. Badala ya kukata tamaa, alianza kufanya utafiti na kutumia Akili Unde (AI) kuchambua mashine zake. Baada ya kurekebisha mfumo wa hewa na mpangilio wa trei, kiwango cha uanguaji kiliongezeka hadi asilimia 81. Teknolojia pia ilinisaidia kupunguza gharama za uzalishaji, Mwendwa akasema. Alianzisha kiwanda chake cha kutengeneza chakula cha kuku kwa kutumia mahindi, soya na malighafi nyinginezo zenye virutubisho, hatua ambayo anasema imepunguza gharama za malisho kwa zaidi ya asilimia 60. Hali kadhalika, Rais huyu wa zamani wa FKF analima Azolla, mmea wa majini ya kijani wenye protini nyingi unaotumika kulisha kuku. Baada ya kukumbwa na kisa cha kukatika kwa nguvu umeme kwa saa nane, aliwekeza katika mfumo wa nishati ya jua ili kuhakikisha mashine za kuatamia zinaendelea kufanya kazi bila kusimama. Licha ya kuwa na zaidi ya kuku 150,000 kwa sasa, Mwendwa bado hajaanza kuuza kwa kiwango kikubwa. "Ninalenga kufikisha kuku 400,000 kufikia Desemba mwaka huu wa 2026 kabla ya kuingia kikamilifu sokoni ili niweze kukidhi mahitaji ya maduka makubwa na wateja wengine," anadokeza. Anachofanya kwa sasa ni kuuza jogoo moja moja. Mradi wake sasa umeajiri wafanyakazi 54 wa kudumu huku Mwendwa akisisitiza kuwa mafanikio yake yametokana na uvumilivu na utatuzi wa changamoto moja baada ya nyingine.
read moretaifaleo.nation.co.ke
@taifaleo Tue, 14 Jul 2026 23:55:33
Njaa yanukia zao la mahindi likikabiliwa na changamoto tele North Rift
WIZARA ya Kilimo imeanza uchunguzi wa kina wa hali ya mashamba ya mahindi katika eneo la North Rift huku hofu ikiongezeka kuwa mavuno ya mwaka huu huenda yakapungua kwa kiwango kikubwa kutokana na ukame uliodumu kwa muda mrefu. Ukame, uhaba wa mbolea ya kukuza mazao na kuongezeka kwa mashambulizi ya wadudu waharibifu vimeathiri maelfu ya ekari za mahindi, hali inayozua wasiwasi kuhusu utoshelevu wa chakula nchini. Maafisa wa kilimo sasa wanatembelea mashamba katika maeneo yanayozalisha mahindi kwa wingi kukusanya taarifa kuhusu maendeleo ya mazao na kukadiria kiwango cha mavuno kinachotarajiwa. Kwa mujibu wa taarifa ya Wizara ya Kilimo, tathmini hiyo inalenga kupima hali ya zao la mahindi lililokuzwa wakati wa mvua ya masika ya mwaka huu wa 2026 na kubaini iwapo uzalishaji utatosheleza mahitaji ya nchi. Waziri wa Kaunti ya Uasin Gishu anayesimamia Kilimo, Sammin Kipkemboi Kottut, alisema wakulima wanapaswa kuwaruhusu maafisa hao kuingia mashambani ili kukusanya taarifa muhimu. Alisema shughuli hiyo ya wiki mbili iliyoanza Jumatatu, Julai 13 itasaidia serikali kupanga hatua za kukabiliana na upungufu wa chakula endapo utajitokeza. Mwaka wa 2024, eneo la North Rift lilizalisha takriban magunia milioni 44.8 ya mahindi na kuchangia mavuno ya kati ya magunia milioni 67 na 70. Hata hivyo, mavuno ya mwaka huu yanatarajiwa kupungua kwa hadi asilimia 30 kutokana na mvua isiyotosha, uhaba wa mbolea na kurejea kwa viwavi jeshi. Katika Kaunti ya Uasin Gishu, mdudu huyo tayari ameripotiwa katika maeneo ya Soy, Moiben na Kapseret. "Mdudu huyu ameripotiwa katika baadhi ya maeneo na tunawahimiza wakulima kutoa taarifa mapema ili wapate dawa za kumdhibiti. Tatizo limeongezeka kutokana na mvua isiyoeleweka," alisema Bw Kottut. Aliongeza kuwa ukame umefanya mazao ya chakula na biashara kunyauka katika maeneo mengi, jambo linalotishia mafanikio yaliyopatikana katika sekta ya kilimo. Wataalamu wa kilimo wanaonya kuwa mdudu huyo ni hatari kwa sababu hushambulia mahindi katika hatua zote za ukuaji wake. Aidha, nondo wa mdudu huyo wanaweza kuruka hadi kilomita 30 kwa usiku mmoja, hivyo kueneza mashambulizi kwa haraka kutoka shamba moja hadi jingine. Mtaalamu wa kilimo kutoka Eldoret, Edwin Lang'at, alisema mabadiliko ya hali ya hewa yamezidisha matatizo ya wakulima. "Mvua isiyotabirika inahatarisha mavuno ya wakulima ambao tayari wameathiriwa na magonjwa," alisema. Katika maeneo mengi ya Bonde la Ufa, mvua imekuwa ya kusuasua tangu Machi, jambo lililoathiri ukuaji na ukomavu wa mahindi. Hali si tofauti katika South Rift. Katika eneo la Trans Mara, Kaunti ya Narok, wakulima wengi walichelewa kupanda mahindi kutokana na ukame uliodumu kwa muda mrefu. Wakulima sasa wanatarajia mavuno madogo, hali inayoweza kusababisha bei ya mahindi kupanda baadaye mwaka huu. Festus Kiprono, mkulima kutoka Ololulunga, alisema mahindi mengi hayakufanya vizuri. "Tunaelekea kupata hasara. Mahindi hayakukomaa vizuri na mavuno hayatatosha hata kurejesha fedha tulizowekeza katika mbegu, mbolea, kukodisha mashamba na kudhibiti wadudu," alisema. Mkulima mwingine kutoka Ntulele, Peter Masharen, aliitaka serikali kuwasaidia wakulima wa mahindi kama inavyowasaidia wakulima wa kahawa. Maeneo ya Rongai na Mauche katika Kaunti ya Nakuru pamoja na Kipkelion, Kericho, nayo yameripoti hali kama hiyo. Katibu wa Wizara ya Kilimo anayeshughulikia Kilimo, Dkt Paul Kipronoh Ronoh, alikiri kuwa mazao yameathirika katika maeneo mengi ya North Rift na South Rift. "Tumebaini kuna uharibifu mkubwa wa mazao. Matokeo ya tathmini yatatusaidia kupanga hatua za kukabiliana na hali hiyo," alisema. Dkt Ronoh alisema iwapo tathmini itaonyesha kuwa uzalishaji wa mahindi hautatosheleza mahitaji ya taifa, serikali itaruhusu uagizaji wa mahindi kutoka nje ili kuzuia uhaba wa chakula.
read morekahawatungu.com
@kahawatungu Tue, 14 Jul 2026 23:32:50
Two arrested in Garissa after police intercept 66 donkeys suspected to be stolen
Two men were arrested in Garissa County after police intercepted two lorries transporting 66 donkeys without ownership documents or movement permits. The suspects were arrested on Tuesday after officers manning the Tana Bridge barrier stopped the two vehicles for inspection. Police said one lorry was carrying 35 donkeys while the second was transporting 31, bringing [...] The post Two arrested in Garissa after police intercept 66 donkeys suspected to be stolen appeared first on Kahawatungu.
read morekahawatungu.com
@kahawatungu Tue, 14 Jul 2026 23:38:37
Body of missing Butere Girls High School teacher found in Kakamega river
Police in Kakamega County are investigating the death of a 32-year-old teacher whose body was recovered from River Sasada, days after he was last seen at his workplace. The deceased was identified as Dickson Muganda, a teacher at Butere Girls High School. According to police, the incident was reported on Tuesday afternoon by a resident, [...] The post Body of missing Butere Girls High School teacher found in Kakamega river appeared first on Kahawatungu.
read moreRight Column Content