kahawatungu.com
@kahawatungu Fri, 17 Jul 2026 01:59:50
Vanna White Net Worth
Vanna White is an American television personality, actress, and former model with an estimated net worth of $85 million. Best known as the longtime co-host of Wheel of Fortune, White has spent more than four decades on television, becoming one of the most recognizable faces in game show history. While she earns a lucrative salary [...] The post Vanna White Net Worth appeared first on Kahawatungu.
read morekahawatungu.com
@kahawatungu Fri, 17 Jul 2026 02:13:58
Chuck Woolery Net Worth
Chuck Woolery was an American game show host, singer, actor, and television personality who had an estimated net worth of $10 million at the time of his death. He built his fortune through a television career spanning more than four decades, hosting some of Americas most popular game shows, including Wheel of Fortune, Love Connection, [...] The post Chuck Woolery Net Worth appeared first on Kahawatungu.
read moretaifaleo.nation.co.ke
@taifaleo Fri, 17 Jul 2026 01:55:22
Wakazi watumia teknolojia kuwakomboa punda 100 walioibwa
WAKAZI wa kijiji cha Kokuro, Kaunti ya Turkana, wameanza kutumia teknolojia ya kidijitali kukabiliana na wizi wa punda na magonjwa ya mifugo, hatua inayobadilisha maisha katika eneo la mpakani mwa Kenya na Ethiopia. Mabadiliko hayo yalidhihirika mwezi uliopita baada ya wavamizi wenye silaha kuiba zaidi ya punda 100. Badala ya kuanza msako wa siku nyingi, wakazi waliripoti tukio hilo kupitia Kituo cha Kidijitali cha Habari za Punda (Donkey Digital Information Hub). Taarifa zilifika haraka kwa maafisa wa usalama na punda hao wakapatikana. Katika eneo hilo, punda ni nguzo ya maisha ya kila siku. Hutumika kubeba maji, chakula, wagonjwa, watoto na mizigo wakati wa kuhama kutokana na ukame. Hapo awali, ukosefu wa mtandao na umbali wa vituo vya serikali ulifanya iwe vigumu kuripoti wizi au magonjwa kwa wakati. Kupitia programu ya Punda Wangu, kila punda husajiliwa kwa picha na alama zake maalumu kama rangi, makovu na michoro ya mwili. Mfumo huo wa kutumia Akili Unde hurahisisha kutambua punda aliyeibwa au kupatikana. Wafugaji wanaweza pia kuripoti wizi, magonjwa au ukatili dhidi ya wanyama kupitia kituo hicho au simu bila malipo, huku maafisa wa usalama na madaktari wa mifugo wakichukua hatua kwa haraka. Mwanafunzi, Nathan Ebei, anasema teknolojia hiyo pia imewasaidia vijana kupata huduma za intaneti na kuwapa wafugaji ushauri wa kitabibu kuhusu chanjo, matibabu na utunzaji wa punda bila kusafiri umbali mrefu. Kwa mujibu wa Takwimu za Kitaifa (KNBS), idadi ya punda nchini ilipungua kutoka milioni 1.8 mnamo 2009 hadi kati ya milioni 1 na 1.17 mnamo 2019. Kupungua huko kunahusishwa na biashara haramu ya ngozi za punda, uchinjaji na wizi unaochochewa na mahitaji ya ngozi hizo katika bara la Asia. Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utafiti Kuhusu Ufugaji wa Kuhamahama (IPDR), Mariko Akileng, alisema mfumo huo unalenga kuunganisha wafugaji moja kwa moja na polisi husika ili kuhakikisha hatua za haraka zinachukuliwa. Pia shirika hilo linaimarisha utekelezaji wa sheria kwa kuwapa mafunzo maafisa wa serikali na wadau kuhusu ulinzi wa wanyama na uendeshaji wa mashtaka dhidi ya wahalifu.
read morekahawatungu.com
@kahawatungu Fri, 17 Jul 2026 01:30:31
How to Buy Dollars with FNB
FNB allows customers to purchase US dollars and other foreign currencies for travel, international payments, and other approved purposes. You can order US dollar cash (foreign notes), load US dollars onto an FNB Multi-currency Cash Passport™, or buy and hold US dollars in an FNB Global Account through Online Banking or the FNB App. Depending [...] The post How to Buy Dollars with FNB appeared first on Kahawatungu.
read morekahawatungu.com
@kahawatungu Fri, 17 Jul 2026 01:34:44
How to Buy Electricity on Capitec Without the App
You do not need the Capitec banking app to buy prepaid electricity. Capitec offers Cellphone Banking through USSD, allowing registered clients to purchase electricity directly from their bank account using any mobile phone. This service is available without an internet connection and is ideal if you do not have a smartphone or prefer not to [...] The post How to Buy Electricity on Capitec Without the App appeared first on Kahawatungu.
read morekahawatungu.com
@kahawatungu Fri, 17 Jul 2026 01:38:18
Stanbic Bank appoints Safaricom executive Michael Mutiga as new Kenya CEO
Stanbic Bank Kenya has appointed Safaricom executive Michael Mutiga as its new Chief Executive Officer, with his appointment taking effect on August 1, 2026. Mutiga, who currently serves as Safaricom's Chief Business Development and Strategy Officer, will take over from Joshua Oigara, who was promoted in February to lead Stanbic Holdings, the bank's parent company. [...] The post Stanbic Bank appoints Safaricom executive Michael Mutiga as new Kenya CEO appeared first on Kahawatungu.
read morekahawatungu.com
@kahawatungu Fri, 17 Jul 2026 01:08:20
How to Buy Bundles on Vodacom
Vodacom offers a wide range of prepaid bundles, including data, voice, SMS, social media, streaming, and combo bundles to suit different communication needs. Customers can purchase these bundles using USSD, the My Vodacom app, VodaPay, the Vodacom website, or participating retailers. Learning how to buy bundles on Vodacom helps you stay connected while managing your [...] The post How to Buy Bundles on Vodacom appeared first on Kahawatungu.
read morekahawatungu.com
@kahawatungu Fri, 17 Jul 2026 01:12:29
How to Buy Data on an FNB SIM Card
FNB Connect allows customers to purchase data bundles for their FNB SIM cards quickly and conveniently. Whether you have a prepaid, top-up, or contract SIM, you can buy data through the FNB Banking App, Online Banking, Cellphone Banking, USSD, or an FNB ATM. Learning how to buy data on an FNB SIM card helps you [...] The post How to Buy Data on an FNB SIM Card appeared first on Kahawatungu.
read morekahawatungu.com
@kahawatungu Fri, 17 Jul 2026 01:24:39
How to Buy Data on a Standard Bank SIM Card
Standard Bank Connect offers flexible data bundles for customers using its SIM cards. Whether you have a prepaid, top-up, or monthly SIM plan, you can purchase additional data through the Standard Bank Connect website or manage your account using the available self-service options. Learning how to buy data on a Standard Bank SIM card helps [...] The post How to Buy Data on a Standard Bank SIM Card appeared first on Kahawatungu.
read moretaifaleo.nation.co.ke
@taifaleo Fri, 17 Jul 2026 00:55:07
Mke mwenza aliyeuguza mume ashinda kesi ya urithi wa Sh200 milioni
MAHAKAMA Kuu ya Mombasa imeamua kwamba, katika hali za kipekee, talaka inaweza kuchukuliwa kuwa ilitokea pale ambapo ndoa imekoma, kwa kuzingatia vitendo vya wanandoa ambao wameendelea na maisha yao tofauti hata kama hakuna amri rasmi ya talaka. Mahakama ilisema ndoa inapaswa kuzingatia hali halisi ya maisha ya wahusika na kwamba ndoa inaweza tu kuendelea kuwepo kwa muda ambao wanandoa wote wanakubali kuendelea nayo. Kulingana na mahakama, kushikilia vinginevyo kunaweza kuifanya ndoa ionekane kama aina ya kifungo gerezani na kukiuka haki ya kikatiba ya ridhaa ya hiari ya kuingia katika ndoa. Uamuzi huo ulitolewa katika mzozo wa urithi wa mali yenye thamani ya zaidi ya Sh200 milioni kufuatia kifo cha Prem Lal Ramnath mnamo Novemba 24, 2019. Mzozo uliwahusisha Bi R.B, aliyedai kuwa mjane wa marehemu, dhidi ya Bi A.G na watoto wake, V.L na Y.G. Bi R.B aliwasilisha cheti kilichoonyesha kuwa alifunga ndoa na marehemu mwaka 1999 Mombasa na baadaye akaomba barua za usimamizi wa mirathi. Alisema aliishi na marehemu kwa karibu miaka 20, akimsaidia katika biashara zake na kumhudumia wakati wa ugonjwa. Pia alitoa figo moja mwaka 2012 ili kuokoa maisha ya marehemu. Hata hivyo, Bi A.G na watoto wake walipinga mchakato huo, wakidai kwamba ndoa ya Kihindu kati ya Bi A.G na marehemu haikuwahi kuvunjwa, hivyo marehemu hangeweza kufunga ndoa nyingine kihalali. Pia walidai kuwa Bi R.B alificha taarifa muhimu na alihusika katika udanganyifu wa kupata usimamizi wa mali. Hata hivyo, ushahidi ulionyesha kuwa Bi A.G alihamia Canada mwaka wa 2001 na hakurejea Kenya hadi baada ya kifo cha marehemu mwaka 2019. Pia ilikubaliwa kuwa marehemu aliishi na Bi R.B wakati wa kifo chake. Mahakama ilibaini kuwa Bi A.G na marehemu walikuwa wameishi mbali kwa miaka mingi, huku Bi R.B akiwa ndiye aliyemhudumia marehemu wakati wa ugonjwa wake. Mahakama ilikataa kubatilisha ndoa ya Bi R.B na marehemu, ikisema alikuwa mke wake na alikuwa na haki ya kuomba urithi bila kuhitaji ridhaa ya watoto wa marehemu. Mahakama pia ilikataa madai kwamba Bi R.B alitoa figo kwa malipo, ikisema hakuna ushahidi wa malipo hayo na kwamba madai hayo yalilenga kuchafua sifa yake. Pia ilikosoa walalamishi kumtaja kwa dharau kutokana na kazi yake ya awali ya kusakata densi, ikisema mtazamo huo unaonyesha ubaguzi wa kitabaka. Kwa kuzingatia hali halisi ya uhusiano huo, mahakama ilisema si haki kwa mwenzi anayemwacha mwenzake kwa muda mrefu na kuishi maisha ya kujitegemea kurejea baadaye na kudai mali ambayo huenda mwenzi mwingine aliitafuta na kuijenga wakati wa kutokuwepo kwake.
read morekahawatungu.com
@kahawatungu Fri, 17 Jul 2026 00:29:28
Justice Muchelule's workers grilled as probe into missing pistol deepens
Court of Appeal Judge Justice Aggrey Muchelule is among six people who have recorded statements with detectives investigating the mysterious disappearance of his firearm, which was later recovered from a slain suspect linked to the high-profile Chaiiwali Café robbery two weeks ago. Among those who recorded statements include family members and domestic staff at the [...] The post Justice Muchelules workers grilled as probe into missing pistol deepens appeared first on Kahawatungu.
read moretaifaleo.nation.co.ke
@taifaleo Fri, 17 Jul 2026 00:21:49
Ol Kalou: DCP ya Gachagua yabwaga UDA ya Ruto
Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) imemtangaza Sammy Douglas Kamau Waweru Ngotho kuwa mshindi wa uchaguzi mdogo wa ubunge wa Ol Kalou baada ya kumshinda mpinzani wake mkuu kwa tofauti kubwa ya kura. Bw Ngotho alipata kura 35,440 huku mpinzani wake mkuu, Muchina Nyaga wa chama cha United Democratic Alliance (UDA), akipata kura 5,460. Afisa Msimamizi wa Uchaguzi, Anthony Njiraini, alitangaza matokeo hayo saa kumi na mbili Ijumaa alfajiri baada ya zoezi la kujumlisha kura lililodumu usiku kucha katika Shule ya Sekondari ya Ol Kalou, mjini Ol Kalou. Ni mgombea huyo wa chama cha Democracy for the Citizens Party (DCP) na maajenti wake pekee waliohudhuria zoezi hilo. Akihutubu kwa mara ya kwanza baada ya kutangazwa mshindi, mbunge huyo mteule alilaani ghasia zilizodaiwa kusababishwa na wahuni wanaoshukiwa kuwa maafisa wa polisi siku ya Alhamisi, hali iliyovuruga upigaji kura katika vituo vingi vya kupigia kura ndani ya mji wa Ol Kalou. "Inasikitisha kwamba tumepoteza maisha kutokana na vurugu hizi za uchaguzi. Mmoja wa waliojeruhiwa, ambaye nilimfahamu vyema na alikuwa mfuasi wangu mkubwa, alifariki kutokana na majeraha yake. Wahuni hao pia waliwashambulia wanahabari wasio na hatia ambao silaha zao pekee zilikuwa kamera, simu na vijitabu. Inauma kwa sababu uhuni huu ulipangwa na kufadhiliwa na baadhi ya wabunge kutoka eneo la Mlima Kenya kwa usaidizi wa maafisa wakuu wa polisi," alisema Bw Ngotho. Alisema ushindi wake mkubwa ni ujumbe wazi kwa serikali kwamba imepoteza uungwaji mkono wa wananchi. "Kilichotokea hapa kinaonyesha yatakayojiri mwaka ujao. Ninaishukuru IEBC kwa kazi nzuri. Ikiwa uchaguzi wa mwaka ujao utaendeshwa kwa namna hii, sina shaka kuwa Muungano wa Upinzani utashinda. Mmeonyesha sisi na Wakenya wote kuwa IEBC ni tume huru kweli," alisema. Pia, aliwapongeza maafisa wa polisi waliovalia sare rasmi, akisema walitekeleza wajibu wao kwa weledi. Kamishna wa IEBC Hassan Noor aliwahakikishia Wakenya kuwa tume hiyo itaendesha uchaguzi ulio bora zaidi mwaka ujao. "Zoezi hili limefanikiwa na tumepata mafunzo muhimu yatakayotusaidia kuboresha uchaguzi ujao. Ninawasihi wanasiasa waelekeze nguvu zao kwa wapigakura, si kwetu. Tuna IEBC moja pekee, na tunafanya kazi usiku na mchana kuhakikisha uchaguzi wa mwaka ujao utakuwa huru na wa kuaminika," alisema kamishna huyo. Seneta wa Nyandarua John Methu, aliyeratibu kampeni za mgombeaji wa DCP, pia alilaani vurugu hizo akisisitiza kuwa waliowashambulia wananchi walikuwa maafisa wa polisi. "Ninamtaka Inspekta Jenerali wa Polisi awakamate na kuwafikisha mahakamani wahuni hawa. Tuna sura zao, taarifa zao na video zinazowaonyesha wakitekeleza vitendo hivyo. Ukiwakamata utakuwa umeitumikia Kenya kwa uadilifu. Usipofanya hivyo, utakuwa umeacha nchi hii kuelekea pabaya," alisema Seneta Methu. Bi Jedidah Muchoki, mwanasiasa kutoka Ndia aliyefuatilia uchaguzi huo kwa niaba ya mgombeaji wa DCP, alisema polisi wanapaswa kuwadhibiti wahuni hao kabla hali haijawa mbaya zaidi. "Tunawashukuru wapigakura wa Ol Kalou kwa jinsi walivyoendesha uchaguzi kwa amani. Uchaguzi ulikuwa wa utulivu hadi wahuni walipoingilia kati. Ushindi mkubwa wa DCP unaonyesha wazi kuwa Wakenya wamechoshwa na serikali hii. Serikali hii haiwezi kujirekebisha na inapaswa kuhudumu kwa muhula mmoja tu," alisema Bi Muchoki, ambaye pia analenga kuwania kiti cha eneo bunge la Ndia.
read morekahawatungu.com
@kahawatungu Thu, 16 Jul 2026 23:53:25
DCP's Sammy Kamau Ngotho declared winner of Ol Kalou by-election
The Democracy for the Citizens Party (DCP) candidate Sammy Kamau Ngotho, was Friday declared the winner of the Ol Kalou parliamentary by-election after garnering 35,440 votes. The Independent Electoral and Boundaries Commission (IEBC) said Kamau defeated United Democratic Alliance (UDA) candidate Samuel Muchina Nyagah, who garnered 5,450 votes. Jubilee Partys Wilson Kigwa finished third. Nyagah [...] The post DCPs Sammy Kamau Ngotho declared winner of Ol Kalou by-election appeared first on Kahawatungu.
read moreRight Column Content