taifaleo.nation.co.ke
@taifaleo 7 hours ago
Wapwani walalamikia ongezeko la vijana kutekwa na kupatikana Nairobi
VIONGOZI na wakazi wa Mombasa wameelezea wasiwasi kuhusu visa vya vijana kupotea, huku baadhi yao baadaye wakipatikana Nairobi na katika viunga vya jiji hilo. Tukio la hivi majuzi lilihusisha wasichana wawili wenye umri wa miaka 16 na 17 ambao waliokolewa wikendi baada ya kudaiwa kuzuiliwa kwa zaidi ya wiki moja. Wapelelezi kutoka Idara ya Kuchunguza Uhalifu (DCI) sasa wanategemea ushahidi wa kieletroniki katika kesi ambapo mwanaharakati Caleb Ngwena anachunguzwa kwa madai ya ubakaji na ulanguzi wa watoto kuhusu kisa hicho. Wasichana hao wawili waliokolewa katika eneo la Kasarani, Nairobi baada ya kutoweka kwa zaidi ya wiki moja. Ngwena alifikishwa katika Mahakama ya Shanzu, iliyowaruhusu wapelelezi kumzuilia kwa wiki mbili ili kukamilisha uchunguzi wao. Mahakama iliagiza azuiliwe katika Kituo cha Polisi cha Mjambere, baada ya kukubaliana na hoja ya upande wa mashtaka kwamba waathiriwa hao ni watu walio katika mazingira hatari na kwamba kumwachilia Ngwena kwa sasa kunaweza kuhatarisha ushahidi na kuingilia kati uchunguzi. "Mahakama imeridhika kwamba polisi wamewasilisha sababu nzito na za msingi za kumzuia Ngwena ili kuwawezesha kukamilisha uchunguzi wao. Ombi hilo limekubaliwa na atazuiliwa katika Kituo cha Polisi cha Mjambere kwa muda wa siku 14," mahakama iliamua. Wasichana hao ni wanafunzi wa Kidato cha Tatu na majirani katika mtaa wa Red Estate, Kiembeni. Walitoweka usiku wa Agosti 25 na kusababisha mama zao kupiga ripoti katika Kituo cha Polisi cha Kiembeni siku iliyofuata. Ngwena alikamatwa nyumbani kwake Kiembeni Septemba 2 na kupelekwa katika Kituo cha Polisi cha Mjambere. Polisi walisema alisafiri hadi Nairobi akiwa ameandamana na maafisa wa DCI Kisauni mnamo Septemba 3 katika juhudi za kuwatafuta wasichana hao. Wasichana hao waliokolewa siku iliyofuata katika eneo la Kasarani, huku wachunguzi wakisema Ngwena alisaidia katika kuwapatia mahali walikokuwa. Wasichana hao waliwaeleza wachunguzi kwamba walichukuliwa kwa nguvu na Ngwena pamoja na mwanamume mwingine usiku walipotoweka. Walisema walilazimishwa kuingia katika gari ambalo hawakulitambua na kusafirishwa kutoka Kiembeni hadi Nairobi, kabla ya kupelekwa Kaunti ya Kiambu. Inadaiwa walifungiwa katika chumba kimoja na kubakwa. Wachunguzi sasa wanafuatilia mawasiliano na ushahidi wa kifedha uliofanyika kabla na baada ya wasichana hao kutoweka. Polisi walisema kulikuwa na mawasiliano mengi pamoja na fedha zilizotumwa kwenda kwenye simu za wasichana hao. Laini za simu walizotumia zilisajiliwa kwa majina ya mama zao. Polisi wanataka kupata taarifa kutoka Safaricom kuhusu akaunti tano za M-Pesa kwa kipindi cha Julai 20 hadi Septemba 6. Taarifa hizo zinajumuisha stakabadhi zilizotumika kufungua akaunti, taarifa za M-Pesa na rekodi za matumizi ya simu. Pia, wanachunguza taarifa za akaunti tatu za Airtel Money pamoja na rekodi zinazohusiana na matumizi ya simu kwa kipindi hicho. Mahakama iliwaruhusu wapelelezi kuchunguza simu nne zilizopatikana, ambazo ni Oppo A9 2020, Samsung Galaxy A04e, Calus W999 na simu ya Nokia. Kitengo cha Polisi cha Kupambana na Ugaidi (ATPU) kimeruhusiwa kufikia simu hizo, kuchunguza yaliyomo na kutoa faili pamoja na programu zilizohifadhiwa kwenye vifaa hivyo. Mpelelezi wa kesi hiyo John Andama, alisema muda wa ziada wa kumzuilia Ngwena ulihitajika ili kupata ripoti za kitabibu za wasichana hao, kuchanganua rekodi za simu na rekodi za fedha, kutoa taarifa kutoka kwenye simu hizo na kurekodi taarifa za mashahidi wengine. Polisi pia walisema Ngwena anawasaidia katika juhudi za kuwakamata washukiwa wengine wanaohusishwa na kisa hicho.Kupitia wakili wake, Ngwena alipinga kuzuiliwa kwake na kuomba aachiliwe kwa dhamana. Upande wa utetezi ulipinga ombi la polisi, ukilitaja kuwa na kasoro za kisheria, huku ukipinga maelezo ya polisi kuhusu safari zake na kukana madai kwamba ndiye aliyewaongoza maafisa hadi Nairobi. "Ni polisi waliompeleka mshtakiwa Nairobi; si kwamba yeye ndiye aliyewaongoza hadi huko," wakili huyo aliambia mahakama. Hakimu alisema polisi wana wajibu wa kutoa sababu za msingi za kuendelea kumzuilia mshukiwa baada ya muda uliowekwa na Katiba. Hata hivyo, mahakama ilisema polisi wamewasilisha sababu za msingi za kuendelea kumzuilia Ngwena, ikizingatia mazingira ya waathiriwa na umuhimu wa kulinda ushahidi. Mbunge Mwakilishi wa Kike wa Mombasa, Bi Zamzam Mohamed, alisema karibu visa 13 vya matineja kupotea vimeripotiwa tangu Agosti. Aliwataka wazazi kuwa waangalifu na kuwa karibu zaidi na watoto wao ili kuzuia visa kama hivyo. "Mambo si mazuri huku nje. Vijana wengi wanapotea, kwa hivyo ninawahimiza wazazi kuwachunga watoto wao kwa makini. Kaeni pamoja na watoto wenu, zungumzeni nao, eleweni changamoto zao," alisema mwishoni mwa wiki iliyopita. Waathiriwa wote wamepelekwa kufanyiwa uchunguzi wa kimatibabu na ushauri nasaha, huku taarifa zikiwa zimechukuliwa kutoka kwa familia zao.
read morekahawatungu.com
@kahawatungu 9 hours ago
Maraga condemns Ruto's crackdown on immigrant small traders
Former Chief Justice David Maraga has criticised the government's crackdown on immigrant small-scale traders, arguing that the enforcement is based on a presidential directive rather than an enacted law. Maraga said the government began enforcing the crackdown on Monday, September 7, following President William Ruto's announcement that hawking and small-scale retail businesses would be reserved [...] The post Maraga condemns Ruto's crackdown on immigrant small traders appeared first on Kahawatungu.
read morekahawatungu.com
@kahawatungu 9 hours ago
TSA launches program allowing non-travelers past security
The Transportation Security Administrationhas launched a new program that allows some people without a plane ticket to go through airport security. The program, called Gateside by TSA PreCheck, allows eligible TSA PreCheck members to enter the secure area of participating airports to meet or see off friends and family at their gate, meet someone during [...] The post TSA launches program allowing non-travelers past security appeared first on Kahawatungu.
read morekahawatungu.com
@kahawatungu 8 hours ago
Menendez brothers granted early parole suitability hearing for March 2027
Erik and Lyle Menendez were granted on Monday an early parole suitability hearing, tentatively scheduled for March 2027. The pair were initially sentenced to life without the possibility of parole for the 1989 murders of their parents, Jose and Kitty Menendez However, relatives of the brothers pushed for years for resentencing and release. Erik and [...] The post Menendez brothers granted early parole suitability hearing for March 2027 appeared first on Kahawatungu.
read morekahawatungu.com
@kahawatungu 8 hours ago
Prince George set for first day at Eton College
Prince George is taking another step in growing up with his first day at Eton College. He is following in the footsteps of his father, the Prince of Wales, who also attended the historic school in Berkshire. The 13-year-old prince will become a boarder at the elite private school, which has taught 20 British prime [...] The post Prince George set for first day at Eton College appeared first on Kahawatungu.
read morekahawatungu.com
@kahawatungu 8 hours ago
Eiffel Tower shut by staff protest after female workers moved for religious visit
The Eiffel Tower was closed on Monday after staff went on strike over female workers being removed for the visit of a Hindu religious group, workers and management said. A delegation of around 100 people linked to the Bochasanwasi Akshar Purushottam Swaminarayan Sanstha (BAPS) group visited the landmark in the French capital on Saturday. Staff [...] The post Eiffel Tower shut by staff protest after female workers moved for religious visit appeared first on Kahawatungu.
read morekahawatungu.com
@kahawatungu 8 hours ago
Trump threatens to stop sale of Canadian Bombardier jets in US
President Donald Trump has warned Canadian aircraft company Bombardier that it can no longer sell in the US unless it moves its manufacturing there. NO MORE SELLING BOMBARDIER IN THE UNITED STATES! Trump wrote in a Truth Social post on Monday. If they want our Market, they must build here, and stop treating America like [...] The post Trump threatens to stop sale of Canadian Bombardier jets in US appeared first on Kahawatungu.
read moreRight Column Content