standardmedia.co.ke
@standard Thu, 16 Jul 2026 05:24:13
High Court lifts three-month jail term against former Nairobi Finance CEC Charles Kerich
Court lifts 3-month jail term for suspended Nairobi Finance CEC Charles Kerich after Sh30m payout to law firm, commits to court-approved plan to clear remaining Sh106m legal fees.
read morekahawatungu.com
@kahawatungu Thu, 16 Jul 2026 04:52:08
Court stops NEMA from enforcing EPR compliance through retailers pending constitutional case
The Environment and Land Court has barred the National Environment Management Authority (NEMA) from requiring retailers to enforce manufacturers compliance with the Extended Producer Responsibility (EPR) regulations until a constitutional petition challenging the directive is heard and determined. In a ruling, the court held that NEMA cannot shift its responsibility of monitoring and enforcing compliance [...] The post Court stops NEMA from enforcing EPR compliance through retailers pending constitutional case appeared first on Kahawatungu.
read moretaifaleo.nation.co.ke
@taifaleo Thu, 16 Jul 2026 04:54:53
Mzozo: Iran sasa yalenga kufunga Bahari ya Shamu
TEHRAN, Iran: BAADA ya kuzima shughuli katika Mkondo wa Hormuz, Iran sasa inaashiria kuwa inaweza kutumia washirika wake, Wahouthi nchini Yemen kufunga Mkondo wa Bab el-Mandeb ambayo ni ya kuingia Bahari ya Shamu. Ikifaulu, Iran itatatiza biashara ya kimataifa na kusababisha bei ya mafuta kupanda hata zaidi. Wachanganuzi wanasema Iran inalenga kuongeza shinikizo kwa Amerika kwa kudhibiti Mashariki ya Kati na Bahari ya Shamu. Mkondo wa Bab el-Mandeb unaunganisha Bahari ya Shamu na Ghuba ya Aden, na ni njia muhimu inayotumiwa na meli nyingi za biashara pamoja na usafirishaji wa mafuta kutoka Saudi Arabia kuenda masoko ya dunia. Jumatatu, afisa mmoja wa ngazi ya juu wa Yemen alionya kuwa majeshi ya nchi hiyo yako tayari kufunga mkondo huo ikiwa Saudi Arabia itaendelea kushambulia Yemen. Alisema hatua hiyo inaweza kusababisha bei ya mafuta duniani kupanda hadi Sh25, 870 kwa pipa. Mohammed al-Farah, mwanachama wa afisi ya kisiasa ya kundi la Ansarullah, maarufu kama Wahouthi, alidai kuwa Amerika inaichochea Saudi Arabia kuendelea na mashambulizi dhidi ya Yemen. Alionya kuwa iwapo hali itaendelea kuwa mbaya, Mkondo wa Hormuz na Bab el-Mandeb zote zitafungwa. Wataalamu wa masuala ya uchumi Mashariki ya Kati wanasema hatua hiyo itaathiri vibaya usafirishaji wa mafuta na bidhaa duniani. Profesa Fawaz Gerges alisema Iran imeonyesha kuwa inaweza kutishia njia zote mbili muhimu za usafirishaji wa mafuta, jambo ambalo litazidisha mzozo wa sasa na kutishia ulimwengu mzima. Wahouthi hapo awali walionyesha uwezo wao wa kuvuruga biashara ya kimataifa. Baada ya vita vya Gaza kuanza mnamo 2023, walishambulia meli katika Bahari ya Shamuwakidai walikuwa wakilenga meli zinazohusishwa na Israel. Mashambulizi hayo yalilazimisha kampuni nyingi za usafirishaji kubadilisha njia na kuzunguka Kusini mwa Afrika, jambo lililoongeza gharama za usafiri. Mtaalamu wa usalama, Andreas Krieg, alisema Iran inaweza kutumia Wahouthi kulemea Amerika iwapo itaendelea kushambuliwa. Naye Abdulaziz Sager wa Kituo cha Utafiti cha Ghuba alisema Wahouthi wana uwezo wa kuvuruga usafiri katika Bab el-Mandeb, lakini huenda wasichukue hatua hiyo bila amri ya Iran. Ingawa hivyo, alionya kuwa jaribio lolote la kufunga njia hiyo linaweza kusababisha Amerika na washirika wake kuanzisha operesheni kubwa ya kijeshi dhidi ya Wahouthi. Vita vinavyoendelea kati ya Amerika-Israel na Iran tayari vimeenea katika sehemu mbalimbali za Mashariki ya Kati, huku maelfu ya watu wakipoteza maisha, wengi wao raia wa Iran na Lebanon.
read morekahawatungu.com
@kahawatungu Thu, 16 Jul 2026 04:43:37
GoVt to distribute over 11,000 assistive devices to learners with disabilities
The Government has announced that it will distribute 11,139 assistive devices to 321 inclusive education programmes and special schools across the country to support learners with visual and physical disabilities. Education Cabinet Secretary Julius Migos Ogamba flagged off the third phase of the distribution exercise at the Kenya Institute of Special Education (KISE) in Kasarani, [...] The post GoVt to distribute over 11,000 assistive devices to learners with disabilities appeared first on Kahawatungu.
read morestandardmedia.co.ke
@standard Thu, 16 Jul 2026 03:20:00
Grade 8 student books bnb with 'lover'; parent sues school, headteacher for suspension
On July 3, 2026, Hospital Hill Comprehensive School management sent home a Grade Eight student and asked her mother to take her for counselling at a government-owned institution
read moretaifaleo.nation.co.ke
@taifaleo Thu, 16 Jul 2026 02:55:53
Mkenya afariki Amerika baada ya gari kutumbukia kwenye bwawa
WAKENYA wanaoishi Amerika wanaomboleza mauti ya Titus Wanjala, aliyefariki baada ya gari alilokuwa akiendesha kutumbukia kwenye bwawa mjini Waukee, jimbo la Iowa. Wanjala, 43, pamoja na raia wa Amerika River Cropper, 23, wote wakazi wa Waukee, walifariki kufuatia ajali hiyo iliyotokea Julai 7. Walioshuhudia tukio walisema gari hilo lilipoteza mwelekeo, likatoka barabarani na kutumbukia kwenye
read morekahawatungu.com
@kahawatungu Thu, 16 Jul 2026 02:24:53
eCitizen services to be unavailable on Saturday night
The Directorate of eCitizen Services has announced that all services on the eCitizen platform will be temporarily unavailable on Saturday, July 18, 2026, to allow for scheduled system maintenance. In a public notice, the Directorate said the maintenance exercise will take place from 7:00 p.m. to 12:00 midnight. According to the Directorate, the planned maintenance [...] The post eCitizen services to be unavailable on Saturday night appeared first on Kahawatungu.
read moretaifaleo.nation.co.ke
@taifaleo Thu, 16 Jul 2026 02:29:39
TAHARIRI: Amani na uwazi ni muhimu katika kura ya Ol Kalou
UCHAGUZI mdogo wa ubunge wa Ol Kalou leo ni zaidi ya mashindano ya kisiasa kati ya vyama na wagombea wa vyama vikuu nchini. Ni fursa ya kuonyesha kwamba, Kenya imejifunza kutokana na makosa ya chaguzi zilizopita na kwamba, taasisi zake zina uwezo wa kusimamia uchaguzi ulio huru, wa haki na wa kuaminika. Hii ndiyo maana Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka Nchini (IEBC) ina wajibu leo wa kuhakikisha kuwa kuna viwango vya juu vya uwazi. Mshindi wa uchaguzi wa leo anastahili kuamuliwa kwa haki wala kusiwe na visa ambavyo vitasababisha kura yenyewe kuzua ghasia au kutiliwa shaka. Maafisa wa IEBC wanapaswa kusimamia zoezi hilo kwa uwazi, uadilifu na kutii sheria. Kila kura itakayoopigwa lazima ihesabiwe kwa uwazi, matokeo ya kila kituo yatangazwe wazi na fomu zote za matokeo zitolewe kwa maajenti na kuwekwa hadharani ili kuondoa mashaka. Wapigakura nao wana jukumu la kutumia haki yao ya kidemokrasia kwa amani. Hawapaswi kuruhusu kushawishiwa kwa pesa, vitisho, propaganda au misimamo ya kisiasa inayochochea chuki. Baada ya kupiga kura hakuna haja ya kumiminika vituoni, bali kila mtu aende nyumbani na kuachia IEBC jukumu la kuhesabu kura. Kukusanyika vituoni na kituo cha kujumuisha kura kutazua tu ghasia na makabiliano kati ya wanasiasa pinzani. Aidha, polisi wana wajibu wa kuhakikisha usalama wa kila mtu bila upendeleo. Maafisa wa usalama wanapaswa kuwalinda wapigakura, maajenti wa vyama, maafisa wa uchaguzi na waangalizi wa uchaguzi. Polisi hawapaswi kuegemea upande wowote wala kutumiwa kuvuruga matokeo ya uchaguzi wenyewe. Hatua yoyote ya kukabiliana na ukiukaji wa sheria inapaswa kufanywa kwa kuzingatia sheria. Ni muhimu pia vyama vya kisiasa na wagombea wakubali kuwa ushindi na kushindwa ni sehemu ya demokrasia. Badala ya kutoa matamshi ya uchochezi au kuhamasisha wafuasi wao kufanya vurugu, wanapaswa kutumia njia za kisheria iwapo watakuwa na malalamishi kuhusu matokeo. Ol Kalou imevutia macho ya taifa kwa sababu uchaguzi huu unatazamwa kama kipimo cha nguvu za kisiasa kuelekea uchaguzi mkuu wa 2027. Hata hivyo, umuhimu wake haupaswi kuwa sababu ya kuvuruga amani au kukiuka sheria. Wakenya wanatarajia kuona uchaguzi unaoendeshwa kwa uwazi, usawa na uaminifu.
read moreRight Column Content